Bilioni 440 kutekeleza mradi wa maji ziwa victoria -simiyu.

 

Waziri wa Maji Jumaa Aweso akishuhudia zoezi la utiaji wa saini kati ya Wizara hiyo na Mkandarasi kutka nchini chini, kwa ajili ya utekelezaji wa mradi mkubwa wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Mkoani Simiyu katika Wilaya za Busega, Bariadi, Itlima kwa awamu ya kwanza na awamu ya Pili Wilaya ya Meatu na Maswa.

    Katibu Mkuu  Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba Pamoja na Mkandarasi kampuni kutoka nchini chini wakipongezana mara baada ya utiaji wa saini utekelezaji wa mradi mkubwa wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwenda Mkoani Simiyu katika Wilaya za Busega, Bariadi, Itlima kwa awamu ya kwanza na awamu ya Pili Wilaya ya Meatu na Maswa.


Na Bahati Sonda, Simiyu.

 

Wananchi wa Mkoa wa Simiyu wanatarajiwa kunufaika na mradi wa maji safi na salama kutoka Ziwa Victoria unaotekelezwa kwa kiasi cha shilingi bilioni 440 ikiwa ni utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na aliyekuwa rais wa awamu ya tano hayati Dkt John Joseph Magufuli.

 

Ikumbukwe kuwa mradi huo umesubiriwa kwa muda mrefu na wananchi wa Mkoa wa Simiyu hatimaye leo wameweza kushuhudia utiaji saini mradi  huo ambao unatekelezwa na Serikali awamu ya sita chini ya Uongozi wa rais Samia Suluhu ambao utakwenda kuzinufaisha Wilaya zote 5 za Mkoa wa Simiyu hivyo kuwawezesha wananchi kuepukana na adha ya upatikanaji wa maji safi na salama.

 

Hayo yamebainishwa mapema leo na Waziri wa Wizara Maji Jumaa Aweso wakati akizungumza na wananchi wa Mkoa wa Simiyu mara baada ya utiaji saini mkataba wa mradi huo ili kazi iweze kuanza na kuwahakikishia wanasimiyu kuwa hakuna mtu yeyote atakayekwamisha mradi huo na kwamba kwa kushirikiana na uongozi wa mkoa watahakikisha unakamilika kwa wakati hivyo kupata huduma hiyo muhimu.

 

Awesso ameongeza kuwa wakati rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akihutubia bunge alitoa maelekezo mahususi kwa Wizara ya maji kuwa wanaokumbana na adha ya maji ni kinamama hivyo hataki kuona wakikumbana na changamoto hiyo na kuongeza kuwa mradi huo utawanufaisha  Wanasimiyu kwenye masuala ya kilimo pamoja na ufugaji.

 

 Aidha Waziri huyo ametoa rai kuwa mradi huo utekelezwe kwa pamoja badala ya kutekelezaa kwa awamu kwani suala la maji halina mbadala huku akiwahakikishia vijana wa Mkoa huo kunufaika na ajira pindi mradi utakapokuwa unatekelezwa.

 

"Tunakwenda kutekeleza mradi huu kwa pamoja sitaki kusikia unatekelezwa kwa awamu ili kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama na yenye kuwatosheleza hivyo kazi yetu sisi viongozi wa Wizara jukumu letu ni kutafuta fedha kushirikiana na wadau wetu na tutafanya kila linalowezekana ili tufikie adhma ya kumtua mama ndoo kichwani na kwamba lengo letu kufikia 2025 upatikanaji wa maji vijijini uwe umefikia 85% na mjini 95%"Amesisitiza Awesso 

 

Awali Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt Yahaya Nawanda amesema kuwa mradi huo ni miongoni mwa miradi mikubwa inayotekelezwa na awamu ya sita na kwamba kwa awamu ya kwanza unatarajiwa kuwanufaisha takriban wananchi 400,000 na kumhakikishia Waziri wa maji kuulinda kwa nguvu zote sambamba kuwahakikishia ushirikiano wakandarasi watakaokuwa wanatekeleza mradi huo.

 

Sambamba na hayo Dkt Nawanda ameeleza kuwa katika bajeti ya mwaka 2023/2024 jumla ya miradi 29 inaenda kutekelezwa kwa thamani ya zaidi ya shilingi milioni 29 kwa hivyo kuongeza hali ya upatikanaji wa maji katika Mkoa kutoka 72% hadi kufikia 79% na kwamba kwa kipindi cha mwaka 1 umefanikiwa kuongeza upatikanaji wa maji 3.78.

 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Mhandisi Nadhifa Kemikimba amesema kuwa lengo la mradi huo ni kuhakikisha wakazi wa Simiyu wanapata maji kwa 100%  serikali hapa nchini kupitia Wizara ya Maji inatekeleza mradi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabia .

 

Aisha ameongeza utapeleka huduma ya maji ya uhakika kwa kuboresha na kupanua mfumo wa usambazaji maji kwenye Wilaya zote na kwamba utahusisha ukarabti na ujenzi wa mabwawa ya kilimo endelevu cha umwagiliaji utakaotumika kupunguza adha ya maji kwa ajili ya kilimo na mifugo na ununuzi wa mbegu bora na uanzishwaji wa mashamba darasa.

Je, una Tangazo, Picha za Matukio, Taarifa au Habari ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi 0746057557 au 0765402289 au Email : simiyupresstz@gmail.com

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post