Na
Derick Milton, Simiyu.
Serikali imesema kuwa mradi wa SHULE BORA unaotekelezwa
katika Mikoa tisa hapa nchini chini ya ufadhili wa serikali ya Uingereza
kupitia mfuko wa UK Aid umeanza kuonyesha mafanikio makubwa katika maendeleo ya
shule.
Mradi huo ambao unatekelezwa katika Shule za Msingi
kwenye mikoa ya Simiyu, Tanga, Pwani, Dodoma, Singida, Mara, Kigoma, Katavi, na
Rukwa unalenga kuunga mkono juhudi za serikali katika kuinua kiwango cha elimu.
Akiongoza timu ya viongozi na watalamu kutoka Wizara ya
TAMISEMI, Wizara ya Elimu, wakiwemo wafadhili wa mradi huo kuangalia utekelezaji
wa mradi huo katika Mkoa wa Simiyu.
Mkurugenzi msaidizi anayeshughulikia Elimu ya watu
wazima Wizara ya TAMISEMI Ernest Hinju amesema moja ya eneo ambalo mafanikio
yamekuwa makubwa zaidi ni kuhimarishwa kwa mpango wa Ushirikiano wa Walimu na
Wazazi Shuleni (UWAWA).
Amesema kuwa mradi wa Shule bora umesaidia sana kukomeshwa
kwa utoro wa reja reja na uliokidhiri kwa wanafunzi, kwani wazazi wenyewe wamekuwa
mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto wote wanahudhuria shule siku zote.
“ Tumetembelea
baadhi ya shule kwenye mkoa wa Simiyu kuangalia utekelezaji wa mradi wa shule
bora, kitu kikubwa ambacho tumekiona na kimekuwa bora zaidi ni kuhimalishwa kwa
mpango wa Umoja wa Walimu na Wazazi (UWAWA), mpango huu umeleta maendeleo
makubwa kwa shule zetu,” amesema Hinju…
“ Tumekuta Wazazi na walimu wamekuwa kitu kimoja, utoro
umekomeshwa, wazazi wanachangia chakula shuleni kwa ajili ya watoto wao, maeneo
mengine wamekarabati madarasa, tumefurahi kuona wananchi wanaona shule kama ya
kwao,” ameeleza Hinju.
Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo katika
Mkoa wa Simiyu, Afisa Elimu Mkoa Majuto Njanga amesema kuwa katika mkoa huo
mradi wa shule bora umefanikisha kuanzishwa na mpango wa utoaji wa chakula shuleni
hasa uji kwa shule zote za msingi mkoani humo.
“ Wazazi wameshirikishwa kupitia kamati za UWAWA kwa
shule zote kwenye mkoa wetu, tumefanikiwa kutoa uji kwa kuanzia, lakini baadhi
ya shule zinatoa na chakula cha mchana, mwitikio umekuwa mkubwa, hii imesaidia
kupunguza mdondoko wa wanafunzi shuleni,” amesema Njanga.
Aidha Afisa Elimu huyo ameeleza kuwa mradi wa shule
bora umesaidia kwa kiwango kikubwa kuwajengea uwezo walimu wa madarasa ya awali
na darasa la kwanza kwa kuwapatia mbinu bora za ufundishaji.
“ Mradi pia umesaidia kuanzishwa kwa vituo vya utayari,
ambapo mpaka sasa tuna vituo 24 mkoa mzima, vituo hivi vimekuwa muhimu sana kwa
jamii, na vimepokea watoto wengi sana ambao walikuwa hawana uwezo wa kutembea
umbali mrefu kufuata shule ilipo,” ameongeza Njanga.
Timu hiyo ikiwa katika shule ya Msingi Sapiwi ‘A’
iliyoko Wilayani Bariadi, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo Henry Kitori amewaeleza
kuwa kupitia UWAWA shule hiyo imefanikiwa kukarabati madarasa mawili ambayo
yalikuwa yamechakaa.
Aidha Kitori amesema kuwa umoja huo umesaidia kuanzisha
mradi wa ufugaji Mbuzi..” tilianza na mbuzi 10, lakini chini ya usimamizi wa
UWAWA tuna mbuzi 31, ambao wanatumika katika maendeleo ya shule yetu”
Mwenyekiti wa UWAWA katika shule ya Msingi Nyakabindi
Elia Shigalu akizungumza mbele ya timu hiyo, amesema kuwa jamii kwa sasa
imetambua umuhimu wa kushiriki katika maendeleo ya shule.
“ Uko nyuma wengi tulidhani shule ni mali ya serikali,
lakini kwa sasa wengi wameelimika kupitia hii UWAWA, tunashirikiana vyema na Kamati
ya shule, shule yetu sasa hivi haina utoro tumekosema, watoto wetu wote
wameanza kunywa uji, tumelima hekari nne kwa ajili ya chakula cha watoto wetu,”
amesema Shigalu.
![]() |
| Mkurugenzi msaidizi anayeshughulikia Elimu ya watu wazima Wizara ya TAMISEMI Ernest Hinju, akizungumza na walimu, wazazi katika shule ya Misngi Nyakabindi, iliyopo Wilayani Bariadi Mkoa wa Simiyu. |


Post a Comment