Na Derick Milton, Simiyu.
Katika
kuhakikisha wakulima wananufaika na mazao yao Taasisi ya Utafiti wa Kilimo
Tanzania (TARI) kupitia kituo chake cha usambazaji wa Teknologia bora za
kilimo(Nyakabindi Hub) kilichopo katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu imetoa
mafunzo kwa wakulima jinsi ya kuongeza thamani kwenye mazao ya mizizi.
Mafunzo
hayo ambayo yalikuwa ya siku moja, yameongozwa na mtafiti mwandamizi kutoka
TARI Ukiriguru Mkoani Mwanza, Dkt. Caresma Chuwa ambapo yamewashirikisha wakulima
zaidi ya 200 wengi kutoka katika Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu.
Dkt.
Chuwa amesema kuwa lengo la mafunzo hayo, ni kuona wakulima wananufaika na
kilimo chao kwa kupata elimu ya jinsi ya kuongeza thamani na siyo kuuza kama
ambavyo wamezoa ambapo wengi wanauza kwa bei ndogo
“
Tunajua kabisa wakulima hasa wa mazao ya mizizi wakivuna wanauza kwa bei ndogo
bila ya kuongeza thamani, wengi hawana hii elimu, kama wadau wakubwa wa kilimo
nchini, tumeona kuja na elimu hii kuwafundisha jinsi ya kuongeza thamani viazi,
pamoja na mohogo, ili wajiongezee kipato,” amesema Dkt. Chuwa.
Amesema
kuwa uwekezaji kwenye kilimo unanzia kwenye mbegu, kanuni bora za kilimo,
kuvuna kwa ufasaha kisha kuongeza thamani ya mazao yenyewe, jambo ambalo ameeleza
wakulima wengi hawafanyi.
“
Kwa elimu hii wengi wameelewa, vyakula na mahitaji yote ya kuongeza thamani
wana uwezo wa kuyapata, hawa ambao tumewapa elimu hii watakuwa walimu wazuri wa
wengine na tunaamini kuwa sasa wakulima watanufaika na kilimo chao,” amesema
Dkt. Chuwa.
Nao
wakulima waliopata mafunzo hayo wameishukuru TARI kwa elimu ambayo wameipata,
ambapo wameeleza kwa mara kwanza waliowengi hawakuwa na elimu ya jinsi ya
kuongeza thamani mazao ya mizizi kama mihogo na viazi.
“
Tunashukuru sana watu wa TARI kwa Elimu hii, wengi nikiwemo mimi hatukuwa na
elimu ya jinsi ya kuongeza thamani mazao yetu hasa viazi, kwa mafunzo haya kama
mkulima naweza kuongeza thamani mazao yangu,” amesema Juliana Mayenga.
Naye
Agness Joseph Mkulima wa Nyakabindi Mbali na kushukuru TARI kwa mafunzo hayo
amewaomba kuendelea kutoa mafunzo kwa wakulima wengine ambao hawakupata mafunzo
hayo.
Mafunzo hayo ambayo yamefanyika jana katika kituo hicho yalilenga zaidi mazao ya mhogo, ndizi, viazi vitamu pamoja na viazi lishe, huku wakulima wakifundishwa pia jinsi ya kupika makande kwa kuchanganya maharage na mbogamboga



Post a Comment