NJALU AONGOZA KURA ZA MAONI ITILIMA KWA 75%.

Njalu Silanga.
 

NA COSTANTINE MATHIAS, Itilima.


ALIYEKUWA Mbunge wa Jimbo la Itilima Mkoani Simiyu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Njalu Daudi Silanga ameshinda kura za maoni kwa kupata kura 8,285 akifuatiwa na Josephine Makongoro aliyepata kura 1822.


Akitangaza Matokeo hayo, Katibu wa CCM wilaya hiyo ambaye pia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi, Joel Makwaia amesema kuwa kura zilizopigwa ni 11, 063, kura halali 10959 na zilizoharibika ni kura 104.


Katibu huyo amewatangaza Wagombea wengine ambao ni  Jeremiah Nkulukulu amepata kura 604 na Emmanuel Subi kura 248.


Mwisho. 





Je, una Tangazo, Picha za Matukio, Taarifa au Habari ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi 0746057557 au 0765402289 au Email : simiyupresstz@gmail.com

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post