Watoto wawili wafariki kwa kula mboga yenye sumu, saba wanusurika kifo.


Watoto wawili wa Familia ya Tandula Ngasa, katika Kijiji Cha Mwakiloba Wilaya ya Busega mkoani Simiyu, wamepoteza maisha na wengine saba kunusurika kifo baada ya kudaiwa kula chakula chenye sumu.


Akiwa kwenye mkutano wa Jukwa la tatu la Ushirika Mkoa wa Simiyu ambapo alikuwa mgeni rasmi, Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Yahya Nawanda amesema kuwa watoto walipoteza maisha mara baada ya kula chakula hicho.


Dkt. Nawanda amesema kuwa watoto wengine saba ambao walinusurika, wamekimbizwa katika Hospitali ya rufaa ya Bugando Mkoani Mwanza kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.


Nawanda amesema kuwa Tandula Ngasa ambaye ni Baba wa Familia alimaka Asubuhi na kwenda alipulizia sumu ya kuua wadudu kwenye shamba la Pamba, ambapo jioni mke wake naye alikwenda kwenye shamba hilo hilo bila ya kujua na kuchuma mboga za majani kwa ajili ya chakula.


“ Mama baada ya kuchuma mboga hizo na kwenda kupika bila ya kujua kama mme wake Asubuhi alipulizia Sumu ya kuua wadudu, walikula mboga hizo ndipo watoto wakaanza kuumwa” amesema Dkt. Nawanda…


“ Watoto wawili walipoteza maisha (hakuwataja majina) lakini wengine saba walikimbizwa hospitali Bugando Mkoani Mwanza, na wanaendelea na matibabu,”


Juhudi za kumtafuta Kamanda wa Polisi mkoa Blasius Chatanda kwa ajili ya kuelezea undani wa tukio hilo zimegonga mwamba, licha ya kupatikana lakini Kamanda hiyo alisema kuwa yupo nje ya Ofisi kikazi hivyo hawezi kuliongelea mpaka arudi kutoka safari.


Je, una Tangazo, Picha za Matukio, Taarifa au Habari ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi 0746057557 au 0765402289 au Email : simiyupresstz@gmail.com

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post