![]() |
| Mkuu wa Wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu Faidha Salim akizungumza wakati wa maazimisho ya siku ya uhuru wa Vyombo vya habari Mkoani humo. |
![]() |
| Katibu Msaidizi wa Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu (SMPC) Derick Milton. |
![]() |
| Mwenyekiti wa Kamati ya Miradi SMPC Mwandishi wa Habari Sitta Tuma. |
Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu (SMPC) kwa kushirikiana na Umoja wa Klabu za waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) jana imeazimishia siku ya uhuru wa Vyombo vya Habari Mkoani humo, ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Mkoa huo Dkt. Yahya Nawanda.
Hafla hiyo ilihudhuliwa na wadau mbalimbali wa Habari mkoani humo, zikiwemo taasisi za kiserikali, wafanyabishara, vyama vya siasa, viongozi wa Dini, waandishi wa Habari pamoja na wafugaji kutoka maeneo mbalimbali mkoani humo.
Akizungumza wakati wa maazimisho hayo, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa ambaye alikuwa mgeni rasmi, Mkuu wa Wilaya ya Bariadi Simon Simalenga aliwataka waandishi wa Habari kuzingatia weledi katika kutoa taarifa zao.
Simalenga alisema kuwa serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa waandishi wa Habari hasa wa Mkoa wa Simiyu, ikiwemo kutatua Changamoto ya upatikanaji wa Bima za Afya ili kuweza kufanya kazi kwa amani.
Awali akizungumza Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu, Frank Kasamwa, aliwashukuru wadau mbalimbali wa Habari Mkoani humo ambavyo wamekuwa wakitoa ushirikiano kwa wanahabari pamoja na Klabu hiyo.






Post a Comment