Rc Simiyu Aimwagia Kongole Bigone Investment kuwekeza Kiwanda cha Pamba.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda (mwenye shati jeusi kulia) akimsikiliza Mmiliki wa Bigone Investment Co. Ltd ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki Stanslaus Nyongo (mwenye reflectore ya mistari) mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda cha kuchambua pamba.

 

Na Mwandishi wetu, Maswa.

 

MKUU wa mkoa wa Simiyu, Dk.t Yahaya Nawanda ameipongeza Kampuni ya BIGONE INVESTMENT Co. Ltd ya Mjini Maswa kwa kuanza ujenzi wa kiwanda ili kuwekeza katika wilaya ya Maswa.

 

Pia amempongeza Mmiliki wa Kampuni hiyo ambaye ni Mzaliwa wa wilaya hiyo, Stanslaus Nyongo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki (CCM).

 

Dkt. Nawanda amesema hayo mara baada ya kutembelea eneo la viwanda lililotengwa maeneo ya Ng'hami mjini Maswa ambalo kampuni hiyo inajenga kiwanda cha Kuchambua Pamba.

 

Amesema kuwa serikali ya mkoa wa Simiyu inawakaribisha Wawekezaji Wazawa na wale wa kutoka nje ya mkoa na nje ya nchi ili waweze kuwekeza katika mkoa huo ambao una fursa nyingi na kwa uwekezaji kama huo unatoka Ajira kwa vijana.

 

Aidha amelitaka Shirika la Ugavi wa Umeme nchini (TANESCO) kuhakikisha linafikisha umeme katika kiwanda hicho ili kitakapokamilika kinaanza kazi mara Moja.

 

MWISHO.

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda ( wa kwanza kushoto) akimpongeza Mmiliki wa Bigone Investment Stanslaus Nyongo (mwenye shati jeupe) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki kwa kujenga kiwanda cha Pamba, kulia ni Mkuu wa wilaya ya Maswa Aswege Kaminyoge.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda ( wa kwanza kushoto) akisikiliza maelezo Mmiliki wa Bigone Investment Stanslaus Nyongo (mwenye shati jeupe) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki, kwa kujenga kiwanza cha Pamba, kulia ni Mkuu wa wilaya ya Maswa Aswege Kaminyoge.

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda ( mwenye shati jeusi kushoto) akimsikiliza Mmiliki wa Bigone Investment Stanslaus Nyongo (mwenye shati jeupe) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki, juu ya ujenzi wa kiwanda cha kuchambua Pamba.

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Dkt. Yahaya Nawanda ( wa kwanza kushoto) akimpongeza Mmiliki wa Bigone Investment Stanslaus Nyongo (mwenye shati jeupe) ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Maswa Mashariki, kwa kujenga kiwanda cha kuchambua pamba, kulia ni Mkuu wa wilaya ya Maswa Aswege Kaminyoge.

 

ukaguzi wa ujenzi wa kiwanda ukiendelea.
 
 
 

Je, una Tangazo, Picha za Matukio, Taarifa au Habari ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi 0746057557 au 0765402289 au Email : simiyupresstz@gmail.com

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post