MrJazsohanisharma

TANKI LA MRADI WA MAJI YA ZIWA VIKTORIA LIKIJENGWA ITILIMA

 

Tanki la Maji lenye ujazo wa lita Mil. 10 linalojengwa katika Kijiji cha Mwasahani wilaya ya Itilima Mkoani Simiyu.


Na COSTANTINE MATHIAS, Itilima.


UJENZI wa Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria unaendelea kutelekezwa Mkoani Simiyu kwa gharama ya shilingi Bil. 440 umefikia hatua mbalimbali ambapo katika wilaya ya Itilima, Mradi huo umefikia asilimia 23.


Wajumbe wa Kamati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Simiyu, wametembelea ujenzi huo katika wilaya ya Itilima na kukagua ujenzi wa Tanki lenye ujazo wa lita Mil. 10.


Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wilaya ya Itilima, Mhandisi Yahaya Hussein amesema baada ya Mradi huo kukamilika itahudumia vijiji 28 na itaongeza upatikanaji wa Maji katika wilaya hiyo kufikia asilimia 95.


"Mradi huu utaruhusu kufanya upanuzi kwenda vijij vingine na pia Tanki kitaruhusu kupeleka Maji wilaya ya Itilima... Mradi huu utafikia wakazi 300,000, Tunamshukuru Rais  Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha za kutekeleza miradi ya Maji." Amesema Mhandisi Hussein.


Diwani wa Kata ya Chinamili, Nindwa Bukanu  amemshukuru Dk. Samia kwa kazi ya kuwaletea Maji na Wananchi wa kata ya chinamili.


Ameeleza kuwa awali walikuwa na shida ya kupata  Maji safi na salama, lakini sasa wanaenda kupata Maji ya uhakika.


Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Eva Ndegeleki amesema Maji ni moja ya vitu endelevu katika Ilani ya CCM ambapo serikali imeweka mkazo ili kuhakikisha wananchi wanapata Maji safi na salama.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Kenan Kihongosi amesema kukamilika kwa Mradi huo kutatua kero ya Maji katika Mkoa huo huku akiwataka wananchi kuendelea kuunga Mkono jitihada za serikali pamoja na kulinza amani.


Amesema ujenzi wa Tanki la lita mil. 10 katika wilaya la Itilima litarahisisha kusambaza Maji katika vijiji 28 vya Itilima.


"Mradi huu uaanzia Busega kuja Bariadi na Itilima, baadae Meatu na Maswa,

Wajibu wetu ni kusimamia Mradi...tunaomba wakandarasi waongeze kazi, thamani ya fedha na Ubora wa Mradi vinaonekana na tumeona vijana wanaozunguka maeneo haya wameajiriwa" amesema Kihongosi.


Mwisho.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Kenani Kihongosi (mbele) akiongoza Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukagua ujenzi wa Tanki la Maji katika wilaya ya Itilima.


Meneja wa Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), wilaya ya Itilima, Mhandisi Yahaya Hussein (kulia) akisoma taarifa ya Ujenzi wa Tanki la Maji linalojengwa Kijiji cha chinamili wilayani humo.


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Kenan Kihongosi (katikati) akizungumza wakati wa kukagua ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka Ziwa Viktoria wilayani Itilima, kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Anna Gidarya.



Katibu wa CCM Mkoa wa Simiyu, Eva Ndegeleki (katikati), akimsikiliza taarifa ya Ujenzi wa Tanki la Maji Itilima, kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Itilima, Mhuli Ngeleja, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Itilima Anna Gidarya.


Tanki la Maji linaendelea kujengwa katika wilayani Itilima.




Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Kenan Kihongosi akiwa na Mkandarasi Mshauri anayetekeleza ujenzi wa Mradi wa Maji kutoka Ziwa Viktoria.



























Je, una Tangazo, Picha za Matukio, Taarifa au Habari ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi 0746057557 au 0765402289 au Email : simiyupresstz@gmail.com

0 تعليقات

إرسال تعليق

Post a Comment (0)

أحدث أقدم